AICC inashiriki maonesho ya 47 Kimataifa ya biashara maarufu kama sabasaba ikieleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kituo. Pamoja kutembelewa na wageni mbalimbali pia imepata nafasi ya kutembelewa na viongozi wa Serikali akiwemo Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambapo ameipongeza AICC kwa kazi nzuri inayoendelea kufanya ya kuileta dunia Tanzania





